SOMA HII RIPOTI YA LEO KUHUSU BEI YA CHAKULA NA CHAI KWENYE BUNGE LA KATIBA, YAANI NI NOOMA




Gazeti la Mtanzania August 28 2014 ndio limeripoti hii stori kuhusu Bunge la Katiba linaloendelea Dodoma, kikubwa ni gharama mbalimbali zinazotumiwa na Wajumbe. 
Wameandika bunge la katiba lateketeza mamilioni ya fedha ambapo kikombe cha chai na biskuti au karanga kinalipiwa shilingi elfu 10 kila siku kwa kila Mjumbe mmoja licha ya kwamba kila Mjumbe anapokea posho ya siku ambayo ni laki mbili na elfu 30.

Kwenye sentensi ya pili wameandika, chakula cha mchana kila Mjumbe analipiwa elfu 16 kwa siku ambapo kwa siku hiyohiyo iendayo kwa Mungu, ni shilingi milioni 8 hulipwa kama gharama za ukumbi wa kufanyia mikutano.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright 2025 EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo