JESHI la polisi hapa nchini limefanikiwa kuwatia mbaroni vinara wa milipuko ya mabomu hapa nchini, Yusufu Ally (30) na mkewe Sumaina Juma (19), wakazi wa Sombetini, wakiwa na mabomu ya kurusha kwa mkono aina ya Gurnet saba, risasi sita za shotgun, baruti, mapanga mawili na bisibisi moja.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa, Mkurugenzi wa 
Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Isaya Mngulu, alisema kati ya mabomu
 hayo moja limetengenezwa nchini Ujerumani na sita yametengenezwa Urusi.
Alisema watuhumiwa hao walikamatwa jana saa 2 usiku katika eneo la 
Sombetini mjini hapa baada ya jeshi la polisi kupata taarifa juu ya 
watuhumiwa hao kuhusika na matukio ya milipuko ya mabomu.
Mtaalamu wa mabomu kutoka Jeshi la Polisi akionyesha kwa waandishi wa habari moja ya bomu lililokamatwa.
  
Aliongeza kuwa polisi inamtafuta kinara muhimu wa mabomu, Yahaya 
Hussen Hela (35), mkazi wa Mianzini jijini hapa, huku watuhumiwa wengine
 25 akiwemo mfanyabiashara maarufu jijini hapa anayemiliki mabasi ya 
Kandahal Said Temba (42), pamoja na Imamu wa Msikiti wa Masjidi Qubia, 
Japhal Lema (38) ambaye pia ni mwalimu wa shule ya msingi wilayani 
Arumeru wakishikiliwa kuhusisana  matukio ya mabomu.
Miongoni mwa watuhumiwa hao, sita kati yao wanahusishwa na tukio la 
ulipuaji wa mgahawa wa Vama uliotokea Julai 7, mwaka huu,na kusababisha 
majeruhi wanane raia wenye asili ya Kiasia.
Watuhumiwa
 sita wa mlipuko huo wametajwa kuwa ni Shabani Hussen (38)ambaye alikuwa
 mlinzi katika mgahawa huo, Mohamed Nuru (30) mlinzi wa mgahawa wa 
jirani na tukio, Japhari Lema (38), Abdul Mohamed (31), wakala wa mabasi
 stand pamoja na Said Temba (42), wote wakazi wa jijini Arusha.
Mngulu alisisitiza kuwa polisi inaendelea kuwasaka wahuhumiwa wengine
 zaidi na kwamba jeshi hilo limeahidi kutoa zawadi kwa atakayeweza kutoa
 taarifa za siri zitakazowezesha kupatikana kwa wahusika hao.
Credit: Global publisher.
Credit: Global publisher.


