SIKILIZA TAMKO LA JESHI LA POLISI KUHUSIANA NA VIUNGO VYA BINADAMU VILIVYOKAMATWA JIJINI DAR


Polisi wa kituo kidogo cha polisi Usalama kilichopo maeneo ya Bunju A Manispaa ya Kinondoni jijini Dar es Salaam jana usiku walilazimika kufyatua mabomu ya machozi pamoja na risasi kutawanya kundi kubwa la wananchi waliokuwa wamekizunguka kituo hicho kwa madai ya kutaka kuwachukuwa watuhumiwa wanaoadaiwa kukutwa na shehena ya viungo vya binadamu.
 
Tukio hilo lililoibua hofu kubwa miongoni mwa wananchi wa maeneo hayo na jiji la Dar es Salaam kwa ujumla, lilitokea majira ya jioni mara baada ya wananchi kushuhudia gari ndogo aina ya Suzuki Carry, ikiwa imebeba viungo hivyo ambavyo vinakadiliwa kuwa vya watu zaidi ya 100.
 
Awali,  kulisambaa taarifa kuwa katika eneo la dampo Mpiji kuna viungo vya binadamu ambapo wananchi walitoa taarifa katika kituo cha polisi Usalama ambapo ufuatiliaji wa tukio hilo ulianza mara moja kabla ya kukamatwa kwa gari hiyo.
 
“Awali tulikwenda kule dampo kwa ajili ya kutupa takataka lakini tuliona viongo vya binadamu tukaja kutoa taarifa polisi na muda mfupi tuliiona ile gari iliyomwaga viungo hivyo ikipita tena kwenda kumwaga vingine na ndipo tulipoifuatilia na bodaboda na baadae kukamatwa na polisi.” Alisema shuhuda wa tukio hilo.
 
Wakaendelea kutabanaisha kwamba, mara baada ya kuona wamezingirwa baadhi ya watuhumiwa walikimbia na kumwacha dereva ambaye alikamatwa na polisi wa kituo hicho cha Bunju A.
 
Mwanahabari wetu ambaye alifika eneo hilo la tukio muda mfupi tangu kutokea kwa tukio, alishuhudia umati mkubwa wa wananchi wa rika mbalimbali wakiwa kituoni hao kwa lengo la kushuhudia tukio hilo.
 
Akizungumza na  waandishi wa habari, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Camilius Wambara, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kubainisha kwamba jeshi lake limekamata viungo hivyo vya binadamu na kwamba tayari wamevipeleka katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa ajili ya uchunguzi zaidi.
 
“Viungo hivyo vimepatikana…Kumepatikiana gloves, kuna visu ambavyo vinatumika mara nyingi katika shughuli mbalimbali za kioparesheni. Viungo hivi ambavyo ni pamoja na miguu, mikono, kuna mafuvu ya vichwa. Kuna mbavu, kuna vitu ambavyo tunadhani inawezekana ni mioyo na vingine ni mapafu. Kwa hiyo tunavichukua na kuvipeleka kule kwenye hospitali ya Muhimbili. Sasa uchunguzi zaidi utafanyika kuanzia hapa.”

Bofya  hapo  chini  Kumsikiliza


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo