SERIKALI YAPEWA "BIG UP" KWA KUYANG'OA MABANGO YA WAGANGA WA KIENYEJI

CHAMA cha Utabibu wa Dawa Asili (ATME) Mkoa wa Dar es Salaam, kimepongeza hatua ya serikali kuanza kuyang’oa mabango ya waganga wa kienyeji na kuomba ushirikiano zaidi, ili kufanikisha zoezi hilo  nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki, Mwenyekiti wa ATME Mkoa wa Dar es Salaam, Rafael Nyampiga, alisema zoezi hilo litakapomalizika jijini Dar es Salaam, waratibu wa ATME, viongozi wa serikali kutoka manispaa zote  watakutana, ili kujadili changamoto na hatua zaidi za kufanya kufanikisha jambo hilo.

Nyampiga alisema zoezi hilo limeanzia kwa sasa limeanzia Wilaya ya Temeke, kubaini waganga 30 wanaofanya kazi kinyume na sheria na kusema kuwa wanaamini kama watashirikishwa vilivyo watakamatwa wengi zaidi.

“Sisi ndio tunaishi na watu hawa na tunajua mbinu zao zote za ufanyaji kazi kwa utapeli, lakini kama mnavyojua sisi wenyewe au serikali yenyewe haiwezi kufanikiwa bila ushirikishwaji wa karibu wa pande zote mbili,”alisema.

Katika hatua nyingine, alikiri baadhi ya namba zinazowekwa kwenye mabango huwa hazipatikani, lakini kwa kutumia wateja wao waganga wanaofanya kazi kwa utapeli ni rahisi kukamatwa.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo