MAJANGA: MICHEZO YA RAGA SABA KILA UPANDE KUPIGWA MARUFUKU, KISA MAADILI YAKE NI AIBU TUPU....!!!!!

Mwenye kiti wa Halmashauri ya kudhibiti vileo  nchini Kenya NACADA  bwana John Mututho ameitaka michezo ya Ragbi ya Masaku 7s kupigwa marufuku na serikali, pia wanamtaka gavana wa machakos DK. Alfred mutua kwa kukubali watoto wadogo kuuziwa pombe wakati wa michezo hiyo.

Msururu wa mechi za raga za wachezaji saba kila upande, hufanyika msimu kama huu kila mwaka na hujumulisha masaku 7s ambayo inaandaliwa katika uga wa Kenyatta mjini Machakos.

Baada ya picha kadhaa kupandishwa kwenye mitandao ya kijamii ikionyesha matukio ya masaku 7s mchana na usiku kucha kumekua na lalama kali kuhusu mashabik kukosa kuonyesha maadili .

Wakati wengine walikua wakiji starehesha kwenye eneo la burudani, msongamano wa magari kati ya mji wa machakos makutano ya bara bara kuu ya Mombasa-Nairobi iliyo chukua masaa 12, baadhi yao wakilala ndani ya gari walipoamka wakajipata kwenye foleni bado.

Matukio yalio wachukiza wengi ni picha zinazo waonyesha mashabik wakiwa wanafanya mambo yasio semeka hadharani na kwa sababu hiyo wakuu kwenye serikali wameanza kutoa hisia zao kuhusu wikendi ya Masaku 7s wa hivi punde zaidi akiwa mkuu wa NACADA.

Mututho analinganisha kilichofanyika kwenye michi hizo za wikendi kuwa yalioshinda Sodom na Gomorrah.

Mwenye kiti huyo wa  Nacada waandalizi wa michezo hiyo walivunja sheria kwa kuruhusu watoto kuuziwa pombe.
Anasema watoto wadogo wenye umri wa miaka  11 waliuziwa pombe kilicho wafanya watake kuchoma kanisa liloko karibu na uwanja huo.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright 2025 EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo