skip to main |
skip to sidebar
WATOTO WAWILI WATEKETEZWA NA MOTO WA PETROLI ILIYONUNULIWA NA BABA YAO HADI KUFA MKOANI PWANI
WATOTO wawili wa familia moja, Nuru (3) na Dora
Kaitaba (2), wamefariki dunia kwa kuungua moto hadi kubaki majivu baada
ya moto mkubwa uliotokana na petroli kulipuka nyumbani kwao, Mapinga,
Bagamoyo mkoani Pwani.
Mtoto Dora Kaitaba (2) wakati wa uhai wake.
Tukio hilo lililowaliza wengi, lilijiri saa tatu usiku, Jumapili iliyopita watoto hao wakiwa ndani na baba yao.
Kwa mujibu wa mashuhuda, baba mzazi wa watoto hao, Kaitaba ambaye ni
mpiga picha wa kujitegemea, alikuwa amerejea kutoka Bunju B alikofuata
petroli ambayo huiuza katika vipimo vidogo vya kwenye makopo ya maji
nyumbani hapo.
Ilizidi kudaiwa kuwa alipofika kwake alishusha mzigo wa mafuta,
watoto wake hao walikuwa wamelala katika kibanda chake cha biashara.
Mtoto Nuru Kaitaba (3) enzi za uhai wake.
Ghafla, mashuhuda wanasema, umeme ulikatika hali iliyomfanya Kaitaba
kuchukua mshumaa na kuuwasha ili andelee na shughuli zake za kuhudumia
wateja.
“Baada ya kuwasha mshumaa, moto huo ulidakwa na petroli hiyo iliyokuwa kwenye dumu na kusababisha mlipuko mkubwa.
Mama mzazi wa wa watoto hao (aliyenyosha mikono) akiwa na simanzi kwa kuwapoteza wanaye.
Mashuhuda walisema Kaitaba alikimbia kutoka bandani, lakini alipopata
akili ya kuwaokoa watoto wake tayari moto ulishakuwa mkubwa na hivyo
kumfanya apige kelele za kuomba msaada.
Mchungaji akiziombea roho za marehemu hao, zikapate kupumzika kwa amani.
Hata hivyo, majirani walishindwa kuingia ndani kutokana na ukubwa wa moto huo na uduni wa vifaa vya kuzimia.
Watu wakiwa wanaangalia tukio hilo kwa masikitiko makubwa, Kikosi cha
Zimamoto Bagamoyo kiliwasili kikiwa kimechelewa hivyo kuambulia kuchukua
majivu ya watoto hao wawili waliaochana mwaka mmoja kuzaliwa.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, SACP Onesphory Matei
amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema tofauti na madai ya
baadhi ya watu kuwa baba mzazi wa watoto hao anashikiliwa na polisi,
alichukuliwa na kupelekwa hospitali kwa ajili ya kutibiwa majeraha na
hatachukuliwa hatua yoyote kwa vile kilichotokea ni ajali.
Aidha
Kamanda Matei alitumia fursa hiyo kupiga marufuku biashara hiyo ya
mafuta ya petroli na dizeli ambayo ni maarufu wilayani humo.
Wakinamama wakipanda gari kuelekea kwenye mazishi ya watoto Nuru na Dora.
Marehemu walizikwa Jumatatu iliyopita kwenye Makaburi ya Bunju, Kinondoni, Dar.
Mungu azilaze roho za marehemu mahali pema peponi, Amina.
CREDITS:GPL
JIUNGE NA EDMO BLOG SASA
Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube
Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi