PICHA; GARI YA MWENYEKITI WA CCM MKOA WA SHINYANGA YAPATA AJALI MBAYA WILAYANI KAHAMA

Gari hilo likiwa eneo la tukio baada ya kuangua na kuharibika vibaya
Gari la Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Shinyanga, Hamis Mgeja, yenye namba T 862 BBC aina ya JEEP, imepata ajali mchana huu katika maeneo ya Nyasubi Kahama, kwenye barabara kuu iendayo nchi jirani za Rwanda na Burundi.
Mwenywkiti wa CCM mkoa wa Shinyanga Hamis Mgeja
Kwa mujibu wa taarifa kutoka eneo la tukio, mara baada ya ajali hiyo dereva wa gari hilo  ambaye hajafahamika mara moja alikimbia, huku ikiarifiwa kuwa alipata majeraha kidogo kwani gari liliangukia upande wake.

Mtu mwingine ambaye alikuwepo katika ajali hiyo hakupata majeraha yoyote, na kwamba Gari hiyo imeinuliwa na kuondolewa eneo la tukio.
Gari hiyo muda mfupi baada ya kuinuliwa kutoka mtaroni
Picha zote na Osward Mabeleea wa farajimfinanga.com


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo