NAIBU MEYA, DIWANI WAPANDISHWA KIZIMBANI KWA SHAMBULIO

NAIBU Meya wa Halmashauri ya Jiji la Arusha, Prosper Msofe (48) na Diwani wa kata ya Levolosi, Ephata Nanyaro (28) jana wamefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Arusha/Arumeru, kujibu mashitaka ya shambulio la kudhuru mwili wa askari mgambo wa Jiji William Mollel.

Akisoma hati ya mashitaka mbele ya hakimu wa mahakama hiyo, Patricia Kisinda, Wakili wa Serikali, Mary Lucas amedai washitakiwa kwa pamoja, Aprili 16 mwaka huu, eneo la Levolosi walimshambulia mgambo wa Jiji la Arusha kwa kumpiga kifuani.

Amedai baada ya kumshambulia wamemsababishia maumivu makali maeneo mbalimbali ya mwili wake. Washitakiwa wamekana mashitaka na wapo nje kwa dhamana baada ya kutimiza masharti.

Hakimu Kisinda amesema washitakiwa hawaruhusiwi kutoka nje ya mkoa wa Arusha isipokuwa kwa kibali cha mahakama


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo