AFP imeripoti kuwa bomu hilo limeripuka katika duka la manunuzi la
Emab Plaza lililo karibu na Banex Plaza, maduka ambayo huwa na wateja
wengi kuliko maduka yote (mall) katika jiji hilo.
“Unaona moshi mkubwa unafuka angani. Ni sehemu ya watu wengi.” Msemaji wa kitengo cha dharura cha Abuja aliiambia AFP.
Ripota wa Vanguard aliyekuwa kwenye eneo la tukio alisikika akiripoti
kuwa anaona vipande vya miili ya watu katika eneo hilo na kwamba bado
kuna watu wafanyabiashara wengi na watu waliotembelea Mall hiyo wamenasa
kwenye jumba hilo.
Zaidi ya ambulance 6 zilionekana zikitoka kwenye eneo la tukio likiwa limejaza majeruhi.