ZITTO KABWE ADAI KESI YAKE IKIISHA MAHAKAMANI ATAWEKA WAZI KAMA YUPO CHAMA KIPYA CHA ACT AMA LAH..!!!

Mh. Zitto Kabwe akihojiwa na clouds fm amesema kuwa hawezi kukubali au kukanusha kama ni mwanachama wa ACT mpaka hapo kesi ya msingi dhidi ya uanachama wake CHADEMA ifanyiwe maamuzi mahakamani.

Kuhusu kauli aliyosema Dr. Kitila Mkumbo kuwa angetamani Mh.ZZK ajiunge na ACT na kugombea uenyekiti wa chama hicho, Zitto amesema kuwa yeye na na Kitila mkumbo wana mlengo wa siasa unaofanana yaani 'social politics' inayoamini katika maendeleo na maslahi ya jamii kwa ujumla na sio chama wala watu wachache.

Amemalizia kwa kusema kuwa kesi yake pindi ikiisha basi atakuwa wa kwanza kuzungumza juu ya chama alichopo.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo