WAUGUZI WAITAKA SERIKALI KUKABILIANA NA TATIZO LA "WAUGUZI FEKI"

CHAMA cha wauguzi nchini tawi la mkoa wa Dodoma, kimeitaka Serikali kukabiliana na tatizo la wahudumu feki ambao wanagushi vyeti na kujihusisha na huduma hiyo. 

Wauguzi hao, wametoa kilio cha leo Mei 16, 2014 wakati wakiongea, kwa masharti ya kutotajwa majina yao mtandaoni (majina tunayo) ambapo wamesema katika baadhi ya Hospitali na Zahanati zilizopo mkoani humo wapo baadhi ya wauguzi wasio na taaluma ya fani hiyo, na kulazimika kuitaka Serikali kuwa na mkakati wa kufanya ukaguzi wa wahudumu na wauguzi ili kuondoa wauguzi wa aina hiyo.
 
Aidha, wamesema hali hiyo inachangia kuwepo kwa lawama kutoka kwa wagonjwa kwa huduma wanazopatiwa na wauguzi wa aina hiyo, kutokana na kukosa maadili ya kazi hiyo.
 
“Wakija hata leo wakikagua watawakamata watu wengi ambao hawajasomea katika fani hii, sisi tunaishauri serikali kuchukua hatua za haraka ili waweze kujua kuwa wanahujumiwa,” alisema mmoja wa wauguzi hao.
 
Hata hivyo, wamesema tatizo la ukosefu wa vifaa vya kutendea kazi katika maeneo yao, umesababisha jamii wanayoihudumia kutokuwa na imani nayo pale wanapo lazimika kuwaambiwa wagonjwa kuwa wakanunue vifaa tiba na dawa kwenye maduka ya dawa baridi.
na FIKRAPEVU 


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo