WANANCHI WANAPOAMUA KUCHUKUA HATUA MATOKEO YAKE NI HAYA

Kufuatia adha waliyokuwa wakiipata wananchi wa kijiji cha Tandala kata ya Tandala wilayani Makete mka wa Njombe wakati wa kuvuka eneo hili, imewalazimu wananchi hao kuchukua hatua na kutumia nguvu zao kujenga daraja hili

Hapo awali mto huu ulikuwa na daraja ambalo lilikuwa limechoka na kusababisha maji kupita juu ya daraja na mengine yakizagaa pembeni na kusababisha wapitaji kushindwa kupita hasa msimu huu wa mvua za masika

Picha zote hapo juu zinaonesha jinsi daraja hilo lilivyojengwa kwa nguvu za wananchi, na kwa sasa maji yanapita muda wote hakuna tena kero

Tazama picha hizi hapa chini uone hali ilivyokuwa mbaya kabla ya wananchi hao kuamua kuchukua hatua


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo