WANAFUNZI MKOANI MANYARA WADAI WANA MAHUSIANO MABAYA NA WAALIMU NDIO MAANA WANAFELI

WAKATI wadau wa elimu wakitupia lawama kwa wanafunzi na wazazi, wanafunzi mkoani Manyara wamewalaumu walimu wao kwa kutokuwa na mahusiano mazuri wawapo shuleni.

Wakizungumza kwenye mkutano wa maadhimisho ya Juma la Elimu za Msingi na Sekondari, baadhi ya wanafunzi walisema walimu wao hasa wa masomo ya Hisabati na Sayansi wamekuwa na tabia ya ukali wanapokuwa darasani, hivyo kuwafanya wafikie hatua ya kuyachukia masomo hayo.

Walisema walimu wao wanashindwa kuwapa msaada pindi wanapotaka kuhoji jambo ambalo halijaeleweka katika somo husika badala yake wanatoa lugha za ukali na kuwakatisha tamaa ya kusoma.

“Mahusiano yetu na walimu wetu hasa wa somo la Hisabati na Sayansi ni mabaya kutokana na wao kuwa wakali na kutufanya tushindwe hata kuuliza maswali, tunaomba wabadilishe mfumo wa ufundishaji, wasiwe wakali ili tuwe karibu nao, pia tuwe huru kueleza shida zetu kwao,” alisema mwanafunzi mmoja wa shule ya sekondari.

Hata hivyo, walibainisha kwamba kuna tabia ya baadhi ya wazazi/walezi wenye watoto wao wanaosoma katika baadhi ya shule wilayani humo kuwakatisha tamaa walimu ambao wamekuwa kipaumbele kufuatilia mienendo ya wanafunzi hao.

Kwa upande wa wadau hao, walieleza wanafunzi wengi wanafeli kutokana na kutokuwa makini na kuzingatia kile walichokifuata shuleni, badala yake wamekuwa wakiendekeza anasa.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo