Marehemu Adam Kuambiana akiwa location enzi za uhai wake.
Hizi ni taarifa zingine za ghafla ambazo Tanzania tumezipokea kwa
mshtuko na masikitiko ni kifo cha miongoni mwa-madirector wa Tanzania
ambao ni waigizaji pia,huyu ni Adam Kuambiana ambaye taarifa za kifo
chake zimeanza kusambaa mchana wa Mei 17.
Mwenyekiti wa Bongo Movie Steve Nyerere amesema>>’Mwenzetu Adam
Philipo Kuambiana amefariki akiwa Location ana shoot,mimi nimepigiwa
simu saa 3 asubuhi kuwa hospitali pale Mwenge niende nikahakikishe kuwa
ni kweli Adam amefariki na kweli kufika pale nikamkuta Adam Kuambiana
amefariki’
‘Sasa hivi tumetoka Muhumbili kwenda kumsitiri mwenzetu,taarifa
inasema wakati yupo location alikua analalamika tumbo linamuuma
linamuuma kumfikisha hospitali ndipo umauti ukamfika’.
Kwa mujibu wa Steve Nyerere amesema kuwa marehemu Adam kuambiana
alikua ana shoot filamu yake mpya ambayo ndani yake amewashirikisha
wasanii kadhaa wa Bongo fleva akiwemo Q Chillah,
