"SIJAWAHI KUTOKA KIMAPENZI NA ROSE MUHANDO NA WALA SITHUBUTU" ASEMA ALEX MSAMA

Mkurugenzi wa Msama Promotions Alex Msama amekanusha vikali taarifa zilizozagaa mitaani kuwa kuwa ana mahusiano ya kimapenzi na mwanamuziki wa nyimbo za Injili Rose Muhando

Msama amesema hana mahusiano yoyote ya kimapenzi na Rose Muhando na wala hajawahi kutembea naye siku za nyuma mpaka leo hii

"Kiukweli nataka kusema mbele yenu hapa. sijawahi kuwa na mahusiano yoyote ya kimapenzi na Rose Mhando, wala msanii yoyote ambaye "ninampromote", hata kumbusu sijawahi, ila nina mahusiano naye ya kawaida tu kama promota wake" amesema Msama

Msama ameyasema hayo kwenye kipindi cha Mkasi kinachorushwa na kituo cha televisheni cha EATV wakati akijibu swali aliloulizwa kuhusu mahusiano yake na Rose Muhando

Amesema suala hilo limemuathiri kiasi kikubwa hasa kwa upande wa familia hivyo kumwambia mkewe ambaye ameathiriwa na taarifa hizo kufanya uchunguzi wa suala hilo na akibaini kuna ukweli yupo tayari kuwajibika kwa hilo


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo