GUMZO LILILOIKUMBA KINONDONI WIKIENDI NI LA KUUAWA KWA MAMBA HUYU



Miongoni mwa stori za mjini  zilizobamba wikiendi  hii ni hii ya Mamba kuuawa Block 41 Kinondoni Dar es salaam kwenye eneo  ambalo wanaishi watu kadhaa maarufu wa Tanzania akiwemo Kalapina wa kikosi cha Mizinga, hii ni nyuma ya bestbite, Mamba huyu akiwa ametokea kwenye bwawa  nyuma ya 41 Records. 
Bwawa limezungukwa na nyumba kwenye eneo la kwa Kisamo zamani Kajima ambapo kwenye hili bwawa zamani kidogo kulikua na Mamba wawili ila baada ya kugundulika mmoja alichukuliwa na watu wa Wanyama ila mwingine hakuonekana.
 
Tukio la juzi ilikua saa nane usiku ambapo mamba huyu alijitokeza barabarani mtaani ndipo majirani wakamuita mtu  mwenye bunduki kwenye huo mtaa ili amuue kwa sababu mwanzoni kabla hawajajua walikua wanahofia kumuua wakidhani ni kosa la kisheria.
 
Baada ya kuuwawa kwa  risasi  nne, Defender ya Polisi ilikuja  na  kumchukua  huyu Mamba


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo