POMBE YAMPONZA ISABELA MPANDA BAADA YA KUVUA NGUO HADHARANI



 
Miss Ruvuma 2006, Isabela Mpanda amedhihirisha jinsi asivyojiheshimu  baada ya kuvua nguo hadharani na kuacha nyeti nje bila kujali watu waliokuwa wakimshangaa.

Tukio hilo la kushangaza lilitokea Alhamisi iliyopita kwenye Ukumbi wa Mawela uliopo Sinza, Dar ambako kulikuwa na kitchen party ya mwigizaji, Vanita Omary ambapo Isabela aliwashangaza watu baada ya kuacha nyeti nje.
 
Bila chembe ya aibu, Isabela akivalia gauni fupi akiwa tilalila, alikuwa akicheza muziki huku akilinyanyua gauni juu na kuacha sehemu nyeti za makalio nje na kusababisha ‘kufuli’ yenye muundo wa bikini kuonekana.

Ishu hiyo ilizua minong’ono kwa baadhi ya wageni waalikwa na kubaki wakimshangaa kwa kitendo hicho....
 
Akiwa anafanya tukio hilo la kujifunua alisikika akisema amepania sherehe hiyo kwani yeye ndiye wifi wa Vanita na kama mwigizaji Jacqueline Wolper aliacha kufuli lake kubwa wazi na yeye aliamua kuonyesha lake aina ya bikini nje ili lionekane kwani ni la bei kubwa.

>>GPL


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo