OFISI ZA GAZETI LA DARAJA LETU ZAVUNJWA, KOMPYUTA NA NYARAKA MBALIMBALI ZAIBWA

Na Mwandishi Wetu, Njombe 

OFISI za gazeti la Daraja Letu zilizopo eneo la Uwanja wa Ndege mjini Njombe, zimevunjwa na kuibwa nyaraka muhimu mbalimbali na kompyuta tano. 

Akizungumzia wizi huo, Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Daraja ambalo ni wachapishaji wa gazeti hilo, Simon Mkina (Pichani) alisema wizi huo uliotokea usiku wa Aprili 30, 2014. 

Alisema kufuatia wizi huo, Jeshi la Polisi Mkoa wa Njombe linawashikilia watu wawili kwa uchunguzi zaidi. 

Mkina akizungumzia mazingira ya wizi huo, alisema dalili zinaonesha kuwa ulipangwa ama na baadhi ya watu wanaojua vyema taratibu za kazi za shirika lake, au watu wenye uhusiano wa karibu na ofisi hiyo. 

"Kuna uwezekano mkubwa wa kuhusika kwa watu wa karibu na shirika letu, lakini kwa kuwa tayari Polisi imeanza kazi zake, ni vyema tukaliacha jeshi hilo likaendelea na matokeo yake tutaambiwa," aliongeza Mkina. 

Mkurugenzi huyo pia alisema huenda asili ya kazi za gazeti lao, hasa habari za uchunguzi ikawa sababu nyingine ya wahusika wa wizi huo wa nyaraka kuhusika. "Siwezi kueleza moja kwa moja iwapo habari zetu za uchunguzi zikawa chanzo pia, lakini sio chanzo cha kupuuza, maana utendaji wetu umekuwa mwiba kwa waendaji wabovu wa halmashauri," alisema Mkina. 

Gazeti la Daraja Letu limekuwa likiandika habari za utendaji usioridhisha wa baadhi ya viongozi wa halmashauri za mikoa ya Njombe na Iringa. kufuatilia matumizi ya fedha na pia kuibua changamoto za maisha na maendeleo kwa mikoa hiyo miwili.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo