BABA MZAZI WA KANUMBA ATOA TUHUMA DHIDI YA MAMA KANUMBA

BABA wa marehemu Steven Kanumba, Charles Kanumba amemshutumu mzazi mwenziye, Flora Mtegoha, kuwa amekuwa na tabia endelevu ya kumtenga kwenye shughuli za mwanaye.

Akipiga stori na waandishi wetu, alisema anamshangaa mama huyo kumtenga mara kwa mara katika ishu za marehemu mwanaye ambapo alitolea mfano wa maadhimisho ya miaka miwili ya kifo cha mwanaye (Kanumba Day) yaliyofanyika hivi karibuni.

“Huenda wana maslahi yao kuamua kulitumia jina la mwanangu, siwezi kuwazuia lakini watambue kuwa wanakosea sana kwa kufanya hivyo bila kunishirikisha mimi baba yake,” alisema baba Kanumba.

VIA GPL


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo