KINACHOENDELEA KWENYE MSIBA WA ALIYEKUWA MKUU WA WILAYA YA KALEMBO MAREHEMU MOSHI CHANG'A


Mkuu wa Mkoa wa Rukwa,Injinia Stella Manyanya akiwa ni mwenye majonzi wakati akisaini kitabu cha Maombolezo ya Kifo cha Mkuu wa Wilaya ya Kalambo, Mhe. Moshi Mussa Chang'a ambae alifariki dunia jana jioni katika Hospitali ya Muhimbili Jijini Dar es Salaam alikokuwa akipatiwa matibabu ya ugojwa wa shinikizo la damu na Kisukari.  

Msiba upo nyumbani kwa Marehemu,eneo la Mbagala jijini Dar es Salaam ambapo taratibu zote zinafanyika hapo.

Taarifa za awali zinaeleza kwamba Shughuli ya kuaga mwili wa Marehemu,Mhe. Moshi Mussa Chang'a itafanyika kesho Aprili 22,2014 nyumbani kwake Mbagala na baadae mwili utasafirishwa kwenda kijijini kwao Mkoani Iringa kwa Mazishi.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,Mh. Said Meck Sadick (katikati) akijadiliana jambo na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa,Injinia Stella Manyanya (kulia) pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Bahi,Mh. Betty Mkwassa wakati wakiwa kwenye Msiba wa Mkuu wa Wilaya ya Kalambo, Mhe. Moshi Mussa Chang'a,nyumbani kwa Marehemu Mbagala,jijini Dar es Salaam leo.
 Baadhi ya Waheshimiwa wakuu wa Wilaya mbali mbali hapa nchini wakiwa kwenye msiba wa Mkuu mwenzao wa Wilaya ya Kalambo, Mhe. Moshi Mussa Chang'a ambae alifariki dunia jana jioni katika Hospitali ya Muhimbili Jijini Dar es Salaam alikokuwa akipatiwa matibabu ya ugojwa wa shinikizo la damu na Kisukari,nyumbani kwa Marehemu Mbagala jijini Dar es salaam.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo