BREAKING NEWS: WAFANYAKAZI WA KAMPUNI YA STRABAG WAGOMA

Wafanyakazi wa kampuni ya ujenzi wa barabara ya magari yaendayo kasi ‘STRATBAG’ wakiwa katika mgomo leo asubuhi.
Mwandishi wa Global TV Online, Patrick Buzohera akiwa mbele ya ofisi ya Meneja Mkuu wa kampuni ya Strabag akijaribu kuzungumza naye, lakini alishuhudia ofisi hiyo ikifungwa mlango na madirisha kabla hajafanya chochote.

WAFANYAKAZI wa kampuni ya ujenzi wa barabara ya magari yaendayo kasi ‘STRATBAG’ iliyopo maeneo ya Ubungo jijini Dar, leo asubuhi wameingia katika mgomo wakipinga uongozi wa kampuni hiyo kuwalipa mishahara midogo wafanyakazi wake na kuondolewa posho zao za wiki na mwisho kabisa wakipinga suala la kutopewa ajira kwa vibarua waliofanya kazi kwa muda mrefu katika kampuni hiyo.

Kamera yetu ilifika eneo la tukio na kuwamulika wafanyakazi wakiwa wamekaa bila kujishughulisha na kitu chochote wakisubiri muafaka kutoka kwa viongozi wao ambao hadi mwandishi wetu anaondoka eneo la tukio hakukuwa na muafaka wowote uliofikiwa baina ya mabosi wa kampuni hiyo na wafanyakazi.

(Picha: Chande Abdallah / GPL)


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo