MADEE AFUNGUKA BAADA YA WIMBO WAKE KUONDOLEWA NA BASATA KUWANIA TUZO ZA KILI 2014

Baraza la Sanaa la Taifa, BASATA limeziondoa nyimbo tatu kwenye mchakato wa tuzo za muziki Tanzania, KTMA kwa madai kuwa zinakiuka maadili ya Kitanzania. Nyimbo hizo ni pamoja na ‘Nimevurugwa’ wa Snura, ‘Uzuri wako’ wa Jux na ‘Tema Mate’ wa Madee.

Madee akizungumza na Bongo5 leo baada ya kupata taarifa ya kuondolewa wimbo wake kwenye tuzo hizo, Madee amesema hajapendezwa na hatua hiyo.
 
“Sichukui hatua yoyote ila nawashangaa tu hao viongozi ambao wanahusika na mchakato mzima. Sisi tunaandika nyimbo ambazo vijana wetu wanazipenda,kwahiyo kama wameamua hivyo basi wawe wanatuandikia wao nyimbo,kwasasabu sisi tunawaandikia vijana wenzetu, sasa unakuta hao wanaoendesha mchakato ni wazee hawawezi kuchanganua maneno yetu,ifike time sasa wawe wanatuandikia mashairi,” amesema Madee.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright 2025 EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo