SAKATA LA BAADHI YA WANANCHI KUGOMA KUTOA MICHANGO YA SEKONDARI YA MLONDWE MAKETE, MWAROBAINI WAKE KUPATIKANA

Mkuu wa mkoa wa Njombe Aseri Msangi(kushoto) akizungumza na waalimu na viongozi wa kata na tarafa kuhusu sakata la baadhi ya vijiji kugoma kuchangia michango ya shule ya sekondari Mlondwe.Kulia ni mkuu wa wilaya ya Makete Josephine Matiro.
 Diwani wa kata ya Mlondwe Alphonce Nkwama akisikiliza maagizo anayopewa na mkuu wa mkoa.
 Mkuu wa mkoa akiendelea na kikao.
 Mkuu wa mkoa wa Njombe akizungumza na wananchi wa kata ya Itundu katika mkutano wa hadhara.
===
Sakata la vijiji viwili vya kata ya Mlondwe kusuasua kutoa michango kwa ajili ya sekondari ya Mlondwe ambayo kwa sasa ipo kwenye kata mpya ya Itundu wilayani Makete limechukua sura mpya baada ya mkuu wa mkoa wa Njombe Aseri Msangi kufanya ziara katika kata hiyo

Kutokana na kusua sua huko mkuu huyo wa mkoa amemwambia diwani wa kata ya Mlondwe Mh. Alphonce Nkwama kuwa anatakiwa kuwaeleza wananchi wake ambao wanagoma kuchangia shule hiyo, serikali itachukua hatua ikiwemo kuwaadhibu wale wote wanaogoma kuchanga

Akizungumza na waalimu na viongozi wa kata na tarafa katika shule hiyo ya sekondari Mlondwe Msangi amesema inasikitisha kuona hatua iliyofikiwa na wananchi ya kuacha kuchangia michango ilihali watoto wao wanasoma shuleni hapo si cha kiungwana hivyo wasipomaliza tatizo hilo, hatua zitakazochukuliwa dhidi yao ni adhabu na wasiilaumu serikali

Amesema mojawapo ya adhabu watakazochukua ni pamoja na kuwatoza ada mara mbili au tatu ya ada ya kawaida inayolipwa na wazazi wanaochanga michango, wazazi wote ambao hawachangi ili iwe fundisho kwao

"hatuwezi kurudishwa nyuma na wananchi wazembe, dawa ni ndogo tu wazazi wote ambao hawachangii watoto wao wakifaulu kuja hapa watalipa ada zaidi, mfano kama mchango ni sh 10000/= wao watalipa 20000/= au 30,000/= au zaidi ya hapo, tuone kama hamtazilipa kwa lazima" alisema Msangi

katika hatua nyingine mkuu huyo akiwa katika kata ya Itundu na Mlondwe alipata fursa ya kuzungumza na wananchi pamoja na kutembelea miradi ya maji iliyopo katika kata ya Mlondwe


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo