MAPAMBANO YA DAWA ZA KULEVYA YAENDELEA IRINGA

 
BIASHARA ya dawa za kulevya mjini Iringa inaendelea kutafutiwa muarobaini, baada ya juzi, jeshi la polisi katika msako wake, kumkamata mtu mmoja akiwa na dawa hizo.
 
Mtu huyo, Vasco Kitosi, alikamatwa akiwa na gramu 50 za bangi ambayo ni aina ya dawa za kulevya inayoelezwa na wanahakati wa mapambano ya matumizi ya dawa hizo, kutumiwa na vijana wengi mjini Iringa.
 
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoani Iringa, Ramadhani Mungi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo linalomuhusisha kijana huyo mwenye umri wa miaka 21.
 
Mungi alisema kijana huyo ni mkazi wa kijiji cha Isagwa kata ya Mlafu, tarafa ya Mazombe, wilayani Kilolo. 
 
source; http:frankleonard.blogspot.com


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo