KITUKO CHAIBUKA USIKILIZAJI WA KESI YA MTUHUMIWA WA MAUWAJI YA MWANGOSI, MWENYEKITI WANAHABARI IRINGA AKAMATWA


 Hapa gari hii  iliyokuwa ikiendeshwa wa WP akisogezwa  ili  kumpakia  askari  mwenzao hamakamani hapo.Picha na habari kwa hisani ya Francis Godwin.

 Hapa  gari  likisogezwa  upande wa  pili baada ya upande  huu kuona waandishi  wametanda na kamera

 Hapa  polisi kanzu  wakijiandaa kufungua mlango  ili kumficha mwenzao

 hapa  wakimuingiza katika  gari huku  wakiwa  wamemfunika usoni kama anavyoonekana wa pili kushoto


 Hapa  wakimsukumiza katika gari  hilo
 gari  hilo likitoka kwa mwendo wa kasi mahakamani hapo likiwa na mtuhumiwa wa mauwaji ya Mwangosi


 Mwanahabari Frank Leonard baada ya  kuachiwa  huru na polisi  leo
.........................
 
WAKATI mahakama kuu kanda ya Iringa ikianza  kusikiliza kesi ya mauwaji ya aliyekuwa mwandishi wa Chanel Ten na mwenyekiti wa chama cha waandishi wa habari mkoa wa Iringa (IPC) marehemu Daudi Mwangosi ,polisi mjini Iringa waanza  kuwanyanyasa  wanahabari wanaofika kufuatilia  kesi hiyo baada ya kumkamata mwenyekiti wao Frank Leonard akiwa ndani ya mahakama wakati kesi hiyo ikiendelea.

Mwenyekiti  huyo alikamatwa  leo majira ya saa 5 asubuhi  wakati jaji  Mary Shangali  akiendelea kumsikiliza wakili wa  serikali Adoph Maganga  ambae  alikuwa akiwasilisha  baadhi ya vielelezo  muhimu  vya kesi  hiyo mahakamani  hapo.

Hata   hivyo katika  hali  iliyowashangaza  wananchi na  wanahabari   waliofika mahakamani  hapo  kusikiliza  kesi hiyo ni baada ya askari  mmoja kusimama ghafla  katika kiti  chache na kwenda kwa wakili wa  serikali na kurudi eneo ambalo wanahabari  walikuwa  wamekaa na  kumsimamisha Leonard  na kwenda kumpeleka kituo  cha  polisi kwa madai kuwa amepiga  picha mahakamani hapo  wakati   jaji akiendelea na kesi jambo ambalo si la kweli.

Akizungumia uamuzi huo  wa askari  hao  kumkamata  Leonard  alisema  kuwa aatambua taratibu zote za  kimahakama na  kuwa asingeweza kupiga  picha  wakati jaji akiendelea na kesi na kuwa  kilichotokea baada ya  kuingia mahakamani hapo kamera  yake  ilikuwa ndani ya mfuko  huku  yeye  akiendelea  kuchukua maelezo kwa  kuyaandika .

Hata  hivyo  alisema wakati  huo  simu  yake aliyokuwa ameiweka mfukoni wakati  akiitoa mfukoni na kutaka  kuiweka  vizuri askari  huyo aligeuka na kuona ameishika simu hiyo na hivyo  kuhisi kama amepiga  picha na kumkamata   na kutaka  kumbambikia kesi ya  kupiga  picha mahakamani  ila baada ya uchunguzi wa awali na maelezo ilibainika si kweli na ndipo alipoachiwa  huru na kutakiwa kuripoti baada ya muda kituoni hapo.

Kabla ya  kukamatwa  kwa  mwenyekiti huyo wa IPC  wanahabari  zaidi ya 10  waliokuwepo mahakamani hapa mapema  majira ya saa 2 asubuhi  walizuiwa  na askari polisi waliomfikisha mahakamani mtuhumiwa wa mauwaji hayo kuwa hawapaswi kuingia mahakamani kusikiliza kesi hiyo kabla ya kufikisha malalamiko hao kwa msajili wa mahakama ambae  alipinga  hatua ya jeshi la polisi kufukuza wanahabari mahakamani  hapo.

Hatua  ya  polisi hao  kumkamata  mwanahabari huyo  iliwalazimu  wanahabari  kumtafuta  kamanda wa  polisi mkoa wa Iringa kwa  njia ya simu ili kuhoji uhalali wa jeshi la polisi kuzuia wanahabari katika mahakama  hiyo na kwakesi hiyo ya askari anayetuhumiwa kufanya mauwaji ya Mwangosi.

Akizungumza kwa  njia ya  simu akiwa safarini kamanda Mungi  alisema polisi hawana mamlaka ya  kuwazuia  wananchi ama  wanahabari  wanaofika mahakamani kwani mwenye mamlaka ya kufukuza ama kuagiza kwa  mtu yeyote anayevunja sheria ndani ya mahakama kukamatwa  ni hakimu ama jaji anayesikiliza kesi na si polisi .

Hata hivyo  wanahabari  hao wameeleza  kusikitishwa na askari  polisi hao  kuendelea  kukandamiza uhuru wa  vyombo  vya habari katika  kesi hiyo ya Mwangosi huku kesi nyingine zikiwemo za  wana siasa  kufikishwa mahakamani kwa  tuhuma za  vurugu  polisi hao  wamekuwa wakionyesha urafiki wa hali ya  juu na wanahabari na hata  kuwapigia  simu ili kufika mahakamani  ila inapofika kesi ya mwenzao huyo  wamekuwa  wakiwageuka  wanahabari na kuwaona adui .

 Mtuhumiwa  huyo ambae   alifikishwa mapema zaidi  kuliko simu nyingine na gari  la polisi akiwa mbele aliondolewa mahakamani hapo kwa  kufishwa  kupita kiasi  na kuingizwa katika gari dogo  binafsi lenye namba T 165 BMP lililokuwa  likiendeshwa na  askari mwanamke (WP) huku vioo vya gari hilo vikiwa haviangazi kwa   ndani  huku  watuhumiwa wawili  wa mauwaji ambao  walikuwa na askari  huyo mahakamani hapo wakipakiwa katika karandinga la polisi.

Msajili wa Mahakama Kuu Tanzania Kanda ya Iringa, Dunstan Nduguru aliwashangaa Polisi kwa kuingia shughuli za mahakama.

"Hata kama mwandishi huyo angekuwa anapiga picha, haikuwa kazi yao kumkamata mpaka wapewe agizo na Jaji Mfawidhi aliyekuwa anasikiliza kesi hiyo," alisema.

Pamoja na askari hao kuwazuia wanahabari kuchukua picha mara baada ya mtuhumiwa huyo kufikishwa mahakamani, Nduguru alisema utaratibu wa mahakama unawaruhusu wanahabari kuchukua picha kabla shughuli kabla shughuli za mahakama hazijaanza na baada ya shughuli hizo kwisha.
 


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo