CHADEMA YASALIMU AMRI ARUSHA, YAWARUHUSU MADIWANI WAKE KUHUDHURIA VIKAO BAADA YA KUVISUSIA MUDA MREFU




KAMATI Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimewataka madiwani wa Mkoa wa Arusha kuhudhuria vikao vya madiwani walivyokuwa wamesusia kwa miaka kadhaa.
 
Imeeleza kuwa kuanzia sasa waanze kuhudhuria vikao hivyo kutokana na wao kuwa wengi na nguvu katika kupinga masuala kadhaa katika vikao hivyo.
 
Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe alisema hayo jana wakati akitoa maamuzi ya kikao cha Kamati Kuu kilichofanyika juzi.
 
Alisema baada ya kuwepo kwa mvutano wa muda mrefu mkoani hapo kamati kuu imeamua kuondoa pingamizi hilo la kutohudhuria vikao vya madiwani katika Manispaa ya Arusha.
 
“Sasa tumewaelekeza madiwani wote wa manispaa hiyo na wabunge kushiriki vikao na kwa kutumia vikao hivyo kusimamia mali za umma na kupinga masuala mbalimbali ndani ya baraza na siyo nje,” alisema.
 
Mbowe alisema Kamati Kuu imeamua hivyo baada ya kuona madiwani wao wamekuwa wengi kuliko vyama vyote vikiungana katika manispaa hiyo jambo litakalosaidia katika kusimamia masuala yao.
 
Mbowe alisema Kamati Kuu imewaagiza madiwani na wabunge kuzungumza na wananchi wa manispaa hiyo na kuwaeleza bayana nia ya kuondoa pingamizi hiyo.
 
“Wanatakiwa kufanya hivyo haraka kwani wananchi wetu hawataki viongozi wao kuhudhuria vikao hivyo ambavyo havina tija kwa maendeleo ya manispaa yao,”alisema.
 
Alisema sasa mapambano yamehamishiwa ndani ya baraza hilo na siyo nje ya ukumbi kama ilivyokuwa hapo awali ili kukabiliana na ufisadi unaofanya katika baraza hilo.

>>Habarileo


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo