BREAKING NEWS: MAAFA YAIKUMBA MAKETE, UPEPO WAEZUA MAPAA YA NYUMBA ZAIDI YA 8 NDULAMO, MAKETE

Habari za kusikitisha kutoka wilayani makete mkoani Njombe zinaeleza kuwa , mvua kubwa iliyoambatana na upepo mkali imesababisha maafa kwa kuezua mapaa ya nyumba zaidi ya 8 zilizopo katika kijiji cha Ndulamo wilayani hapo majira ya saa 10 jioni ya leo

Kwa mujibu wa ripota wa mtandao huu wa eddymoblaze.blogspot.com aliyefika eneo la tukio baada ya kupigiwa simu na wananchi hao, amesema haijafahamika mara moja kama tatizo hilo limesababisha vifo ama madhara makubwa kiasi gani

Mwandishi huyo ameshuhudia mabaki ya vipande vya mabati yaliyokuwa yamekwama juu ya miti iliyopo jirani na eneo hilo 

katika hali iliyoacha watu wengi midomo wazi, mapaa yaliyoezuliwa katika nyumba hizo hayajaonekana eneo la tukio licha ya kuonekana vipande vya mabati peke yake lakini si mbao

Kufuatia hali hiyo, mbunge wa Makete ambaye ni waziri wa nchi ofisi ya makamu wa rais - mazingira Dkt Binilith Mahenge amefika eneo la tukio na kujionea hali halisi huku akitoa kiasi cha shilingi 100,000/= taslimu kisaidie wahanga wa tukio hilo

Dkt Mahenge ambaye ameambatana na viongozi mbalimbali wa wilaya wakiwemo mwenyekiti wa CCM wilaya ya Makete wameonesha kuguswa na tatizo hilo huku nao wakitoa michango yao kwa wahanga wa tukio hilo

Amewaahidi kuwa serikali itatathmini tatizo hilo mara moja na pia kiasi cha fedha kutoka kwenye mfuko wa jimbo kwa ajili ya maafa hayo kitatolewa kusaidia walioguswa na tatizo hilo

taarifa zidi utazidi kuzipata hapa hapa ikiwemo picha za tukio hilo, tunaomba uwe na subira mpendwa msomaji wetu


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo