WANANCHI WA IRINGA WATAKIWA KUWEKA MAZINGIRA SAFI KUEPUKA MAGONJWA

Wananchi katika manispaa ya Iringa wametakiwa kuweka mazingira katika hali ya usafi kwa kipindi hiki cha msimu wa mvua, ili kuweza kuepuka magonjwa mbalimbali ya mlipuko.

Hayo yamesemwa na Afisa afya wa manispaa ya Iringa, MERCY KINENEKEJU ,na kusema kuwa wananchi wanatakiwa kufanya usafi nje ya makazi yao na kutupa taka sehemu husika.

KINENEKEJU ameongeza kuwa kutokana na changamoto waliyonayo ya magari ya kubebea taka, wanafanya jitihada za kupata magari kupitia mradi wa Word  Bank ifikapo FebruarI mwaka huu watapata msaada wa gari moja ili kupunguza mlundikano wa taka katika baadhi ya maeneo.

Wakati huohuo ameviomba vyombo vya habari kuzidi kutoa elimu kwa wananchi juu ya usafi wa mazingira ili kuweka manispaa katika hali ya usafi.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo