WAKAZI WA IRINGA WAOMBWA KUWACHUKIA VIBAKA NA KUWAFICHUA KUSHIRIKIANA NA JESHI LA POLISI MKOANI HUMO

Wananchi mkoani Iringa wameombwa kuwachukia vibaka na kuwafichua kwa kushirikiana na jeshi la polisi kulinda usalama wa mkoa kwa kuwadhibiti na kuwamaliza .

Hayo yamesemwa na kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Iringa, RAMADHAN MUNGI  na kusema kuwa vibaka hao wanafahamika na endapo wananchi watawafichua watasaidia kuwadhibiti na kuwafanya wafanyabiashara na wananchi kuishi kwa usalama.

Kamanda amesema kuwa jeshi la polisi linaupungufu wa polisi na maeneo mengi yanavibaka, hivyo linahitaji msaada wa wananchi katika kutenda kazi kwani bila ushirikiano wao hawataweza kuwadhibiti.

Hata hivyo amesema kuwa kwa ushirikiano huo kutasaidia kuweka mikakati ya kuzuia uhalifu katika mkoa ,kwani kwa kufanya hivyo kutasaidia kutunza amani ya nchi yetu.

Aidha ameongeza kwa kusema kuwa hali ya usalama katika mkoa wa Iringa ni nzuri kwa sasa na uhalifu unazidi kupungua huku akisisitiza ushirikiano ili kulinda usalama.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo