MJAMZITO ANASWA NA POLISI AKIDAIWA KUFANYA UKAHABA

Stori: ISSA MNALLY NA DUSTAN SHEKIDELE
OPARESHENI ya Polisi wa Mkoa wa Morogoro na kikosi maalum cha kufichua Maovu cha Magazeti ya Global Publishers (OFM), imemnasa mwanamke mjamzito katika kamatakamata ya machangudoa.

 
Polisi akimkagua changudoa mwenye mimba aliyenaswa akijiuza.

Katika oparesheni hiyo ya aina yake iliyofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita katika eneo la Msamvu (Kambi ya Itigi), wanawake 30 waliodaiwa kujihusisha na biashara hiyo walikamatwa.

Waandishi wetu wakiwa na askari wa mkoa huo walimnasa mjamzito huyo anayedaiwa kuwa na mimba ya miezi sita akiwa mawindoni eneo hilo.
Changudoa huyo mwenye mimba akiwa chini ya ulinzi.

Mara baada ya mjazito huyo kukamatwa alitoa yake ya moyoni kwa kusema kwamba anafanya biashara hiyo ili kupata fedha za kujikimu na ujauzito wake haumpi shida yoyote.

“Jamani natafuta pesa za kujikimu na maisha hapa mjini sasa mnatukamata tukale wapi? Hii mimba ni yangu na ninayefanya ukahaba ni mimi niacheni,” alisema mdada huyo.

Pamoja na maneno yake, polisi walimbeba msobemsobe na kumfikisha kituoni pamoja na makahaba wengine.

CREDITS; GPL


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo