WAKAZI WA WILAYA YA MAKETE WASHAURIWA KUJENGA DESTURI YA KUSOMA VITABU

Wananchi wilayani Makete Mkoani Njombe wametakiwa kujijengea utaratibu wa Kujisomea Vitabu Mbalimbali  kwani ni Njia Moja wapo yakuongeza Maarifa.

Kauli hiyo imetolewa na Askofu mstafu wa Dayosisi ya kusini Kati Dkt Solomon Swalo (pichani)katika Tafrija ya kumpongeza baada ya kutunukiwa shahada ya Uzamivu (PHD) iliyofanyika Bulongwa Makete

Dk Swalo ambaye pia ni mwandishi mahili wa vitabu amesema amekuwa akiandika vitabu mbalimbali kwaajili ya kuweka kumbukumbu ya vizazi vilivyopo na vijavyo lakini hakuna wasomaji wa vitabu hivyo.

Akizungumza kwaniaba ya Serikali Mkuu wa Wilaya ya Makete mh. Josephine Matiro Amesikitishwa natabia ya Baadhi ya watu na Tabia ya kuto kupenda kusoma Vitabu na kuwataka wananchi kuanza kujisomea.
mh. Matiro amesema kuwa serikali ipo pamoja na kanisa ili kujiletea maendeleo Hivyo anaimani mchango wa Askofu Mstaafu Dk Swalo Unahitajika sana katika Jamii.

Katika Hatua nyingine kanisa limempa Hati ya Jengo Askofu Dk Swalo kwa ajili ya kuuzia Vitabu lililopo Eneo la Namanga Bulongwa.

Tukio Hilo la Kumpongeza Dk Swalo limehudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa Serikali, kanisa pamoja na wananchi.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo