WAFANYABIASHARA NA ABIRIA WALALAMIKIA KERO YA KITUO CHA IPOGORO - IRINGA.

Baadhi ya Wananchi wanaoishi katika manispaa ya Iringa wameiomba Serikali kukarabati eneo la stendi ya Ipogoro kutokana na mazingira ya eneo hilo kutoridhisha, hususaN  kipindi hiki cha mvua.

Wananchi hao wameyasema hayo leo walipokuwa wakizungumza ana kwa ana na mshika kalamu wa hapa jamvini,aliyefika eneo la tukio,na kujionea hali halisi ya eneo hilo ambalo limeonekana kuwa kero kwa wakazi wake.

Baadhi ya Wananchi ambao ni Wafanyabiashara wa eneo hilo wamesema kuwa mara kadhaa wamekuwa  wakidaiwa ushuru  kwa ajiri ya kuboresha eneo hilo,lakini wanashangaa hakuna linalofanyika katika kuboresha stendi hiyo.

Aidha wameitaka serikali kuboresha miundombinu ya eneo hilo la stendi ya ipogoro ili kuraisisha utendaji kazi wa Wafanyabiashara hao na wakazi wengine wa eneo hilo kwa ujumla sambamba na watumiaji wa kituo hicho a.k.a abiria.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo