KAMPENI ZA UCHAGUZI MDOGO IRINGA KUANZA KESHO,JESHI LA POLISI LATOA TAHADHARI SUALA LA VURUGU

Kufuatia kampeni za uchaguzi mdogo ambazo zitaanza kesho Chama cha mapinduzi  (CCM), kimesema kuwa kimejiandaa vizuri na kinauhakika wa kuchukua nafasi hiyo.  
Akizungumza na katibu wa CCM mkoa,Bwa Mtenga Husein amesema kuwa kura za maoni kwa wagombea zimefanyika leo na  wagombea wanakabidhi fomu hii leo katika kata ya Nduli.

Katibu amewataka wanachi kumchagua kiongozi atakayewaletea maendeleo na si kufuata chama anachotoka,hii itapelekea kuwasaidia wananchi kumpata kiongozi  mwenye uadilifu, makini na mwenye kujituma katika suala zima la kuleta na kujenga maendeleo kwa Wananchi wake halikadhalika kwa maendeleo ya Taifa kiujumla.


Kwa upande wa jeshi la polisi,akizungumza kamanda wa Mkoa wa Iringa Ramadhani Mungi,amewaonya wanasiasa wote ambao watajinadi kuwania nafasi hizo kutumia lugha nzuri na zenye staha katika suala zima la kulinda amani na utulivu kwa kipindi chote cha kampeni.Aidha ameongeza kwa kusema kuwa kwa yoyote atakayetumia lungha itakayosababisha kuvunja amani hawataweza kumvumilia.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo