UBOVU WA BARABARA ENEO LA VIWANDA VYA KUSAGA NA KUKAMUA MAFUTA ENEO LA SIDO MBEYA NI KERO KWA WAFANYA BIASHARA ENEO HILO

 Hapa ndio hapapitiki kabisaaaaaa,ni bwawa la samaki.
 Kwa mbali nafaka zikiwa zimetunzwa huku maji yakiwa yamezunguka eneo hilo.
 Barabara ikiwa tope tupuuu hivyo kufanya ushushaji wa nafaka kuwa mgumu.
Hali ya barabara katika eneo la sido mkoani Mbeya ni ya kutisha na kuhuzunisha sana. Eneo hilo ambalo limetengwa maalumu na Jiji la mbeya kwa ajili ya stoo za wafanyabiashara na pia ni maalumu kwa watu wanaohusika na ukoboaji, usagaji na kukamua mafuta ya alizeti.

Ukifika eneo hilo kipindi cha kiangazi huwa ni kavu lakini kuna mashimo mengi yasiyorekebishwa.
Shida huwa inakuja kipindi cha masika na mvua nyingi ambapo kupitika kwa maeneo yanayozunguka eneo hilo huwa ni shida sana kwa waenda kwa miguu na pia magari makubwa na madogo yanayoshusha na kupakia mizigo kutoka sehemu mbali mbali za Tanzania.

Eneo hili pia ni kiungo muhimu sana kwa wakazi wanaokaa maeneo ya uwanja wa ndege, kwa kuwa wengi wanatumia njia hii kama ni shortcut ya kufika haraka majumbani mwao.

Dj sek blog ilifanya uchunguzi yakinifu kwa takribani wiki moja eneo hili na kuweza kuvumbua mambo mengi sana,Moja ya mambo hayo ni kwamba kwa kiasi kikubwa eneo hili hutumika kama makazi yasiyo rasmi kwa watoto wa mitaani,ambao wengi hawana makazi au mahala pa kulala.
Watoto hao wa mitaani hutumia majengo ambayo hayajamalizika vizuri kujiihifadhi kama makazi yao,Mtandao wetu ulifanya mahojiano na baadhi ya wamiliki wa mashine na stoo za eneo hilo kubwa ni kutaka kujua kwa nini eneo hilo limetawaliwa na madimbwi,mashimo makubwa na maji yaliyotuama kwa wingi.

Wafanyabiashara hao wameitupia lawama uongozi wa jiji kwa kushindwa kusimamia vizuri eneo hilo ambalo limetengwa maalumu kwa ajili yao, wakiongeza kuwa wanatoa kodi kila mwaka,kila mwezi walitegemea kodi zao zitatumika kukarabati eneo hilo lakini kinyume chake imekuwa ni shida kwao.

Wafanyabiashara hao wameeleza kuwa magari yanayokuja kushusha na kupakia yamekuwa yakipata sana shida kupita eneo hilo hasa kipindi kama hiki cha mvua,hivyo wameiomba Serikali kuwasaidia kukarabati eneo hilo.

Mtandao huuu ulijaribu kumtafuta mtu anayeratibu na kusimamia eneo hilo lakini mpaka tunamaliza utafiti huu hatukuweza kumpata.Rai ya mtandao wetu ni kwamba viongozi msikae tu huko maofisini tokeni nje pia huku muone wanaicni wanavyokuwa na kero nyingi.
(PICHA NA DJ SEK BLOG)


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo