TAZAMA PICHA 12 ZIKIONESHA HALI ILIVYOKUWA MAHAKAMANI BAADA YA ZITTO KABWE KUSHINDA KESI

 HONGERA: Wakili wa CHADEMA Tundu Lisu (kulia) akilazimika kumpongeza aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA, Zitto Kabwe baada ya Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam, John Mkamwa, kuridhia zuio la Zitto asijadiliwe na ngazi yoyote ya maamuzi ya Chadema, hadi kesi ya msingi aliyofungua dhidi ya chama hicho itakapomalizika. Jaji huyo amekubali kesi ya msingi iungurume na itaanza kusikilizwa Februari 13, mwaka huu.
 Zitto akitoka kwa msaada wa mabaunsa wake katika chumba cha mahakama kuu baada ya uamuzi huo wa  Mahakama kuu leo jioni.
Tundu Lisu na wapambe wake wakionekana kutoka kwa aibu Mahakamani baada ya kubwagwa
 Tundulisu akizungumza na waandishi nje ya mahakama
 Wakili wa Zitto akizungumza na waandishi nje ya mahakama kuu
 Wafuasi wa Chadema wanaomuunga mkono Zitto wakishangilia abaada ya ushindi wa kiongozi huyo
Wafuasi wa Chadema wanaomuunga mkono Zitto wakiwa wamekaa chini kutii amri ya polisi baada ya matokeo ya kesi kutangazwa upende wao ukiwa aumeibuka kidedea
 Wafuasi wa Chadema wanaounga mkono uongozi wa chama hicho kutaka Zitto atimuliwe uanachama, wakiwa wameduwaa nje ya mahakama baada ya uamuzi wa Jaji, John
 Mmoja wa wafuasi wa Chadema upande wa wanaounga mkono uongozi akiwa amejeruhiwa kichwani baada ya kupigwa jiwe.
Mbwa mkali wa polisi akiwa tayari kwa lolote.
 Wafuasi wa Chadema wakivurumishana mawe Zitto alipowasili mahakamani
Wananchi wa kawaida wakilazimika kusalimisha maisha yao kwa kutimua mbio baada ya wafuasi hao wa Chdema kuanza kuvurumishiana mawe Zitto alipowasili Mahakama kuu.Picha zote na the nkoromo blog


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo