MCHAWI ADONDOKA USIKU WA KUAMKIA LEO WILAYANI KAHAMA MKOANI SHINYANGA…!!


Kikongwe huyo akiwa chini huku amezingirwa na kundi la wananchi

Kikongwe mwenye umri kati ya miaka 85 hadi 90 ambaye bado hajafahamika jina lake amekutwa katika kijiji cha Nyashimbi kata ya Muhongolo wilayani Kahama Mkoani Shinyanga kwa kile kinachodaiwa kuwa huenda ni mchawi aliyeanguka usiku wakati akiwa kwenye
safari zake angani.

Kikongwe huyo baada ya kufikishwa kituo cha polisi
Kwa mujibu wa wakaazi wa Kijiji hicho bibi huyo ameonekana leo majira ya saa 12 asubuhi akiwa katika vichaka vilivyo kando ya barabara na alipoulizwa aliongea kidogo tu kuwa anatoka Kijiji cha Nyihogo wilayani Kahama.

Akiwa amelala chini kwa kile kinachodaiwa ni njaa
Alipoendelea kuhojiwa alisema alikuwa na wenzake na vitu mbalimbali ila wamemuacha, huku akisema hawezi kuongea zaidi kwani anahisi njaa kwakuwa alikula toka jana tena chakula Kibichi, jibu ambalo liliwashangaza wengi ni aina gani ya chakula ambacho huliwa kikiwa kibichi.

Bibi huyo amekutwa na nguo moja ya Kimasai na nguo zingine chache za kawaida lakini hakukutwa na vitu vyovyote vinavyoashiria kuwa huenda ni mchawi, hivyo kuleta hisia kuwa huenda alikuwa ni mtembea kwa miguu tu aliyepotea njia kwani watu wote wa eneo hilo hakuna anayemtambua.
 
chanzo:dunia kiganjani


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo