NIKKI WA PILI AKANUSHA KUTOA WIMBO UITWAO NGALELO


_MG_0023
Msemaji wa Weusi, Nikki wa Pili amekanusha kuachia wimbo unaoitwa ‘Ngalelo’ ambao umeonekana kwenye baadhi ya blogs kama wimbo mpya wa rapper huyo.

 “Kuna wimbo nimeona wametoa toa kwenye mablog wameandika kwamba nimetoa wimbo wangu mpya, of course huo sio wimbo. Kuna studio nilikuwa nimeenda nikafanya freestyle tu inaonekana hao jamaa wameivujisha.” Nikki wa Pili ameiambia tovuti ya Times Fm.

“Ni ile ile (studio) ya Afro Centric lakini ni producer mwingine na sio producer ambaye yuko sasa hivi. Ni kule maeneo ya Hostel karibu na chuo kwa hiyo nilikuwa na shindashinda hapo.” Ameeleza Mweusi.

Hata hivyo, mkali huyo wa ‘Good Boy’ amesema kuna baadhi ya mistari katika hiyo freestyle iko katika nyimbo zake.
“Kuna baadhi ya mistari iko katika ngoma zangu nyingine, lakini kwa kuwa wamelikisha mi naona sio issu, mimi mashairi kwangu sio issue.”
Jana (January 3),Nikki wa Pili aliiambia tovuti ya Times Fm kuwa yeye na Joh wataachia wimbo wao wa pamoja February.
Source: http://timesfm.co.tz


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo