MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MAKETE AJIBU KERO ZA WANANCHI WAKE

Wananchi wilayani Makete mkoani Njombe wameelezea changamoto mbalimbali zinazowakabili kwa mh. Daniel Okoka ambaye ni mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya hiyo zikiwemo, maji, umeme, barabara, elimu, pamoja na matangazo ya redio

Kero hizo zimetolewe usiku wa kuamkia leo katika kipindi maalum cha Twanga swali Kitulo FM kinachorushwa na redio kitulo fm chini ya udhamini wa gazeti la daraja jana saa 1:15 hadi saa 3:20 usiku

Akijibu swali kuhusu elimu mh Okoka amesema wananchi wengi wamekuwa na mwamko mdogo kuhusu elimu kwani miongoni mwa wazazi wamekuwa wakishiriki kuwapeleka watoto mijini kufanya kazi mbalimbali badala ya kuwapeleka shule

Kuhusu miundombinu ya barabara kwa kiwango cha lami kutoka Njombe - makete amesema jitihada kubwa zimeshafanyika na kwa sasa upembuzi yakinifu umeshafanywa makete mjini na mara baada ya kumalizika kipindi hiki cha mvua za masika ujenzi utaanza mapema

Kwa upande wa umeme hasa kwa kata ya Tandala Okoka amesema nguzo tayari zimeshasimikwa, nyaya na transfoma nazo yatari zimewekwa hivyo kwa sasa kilichobakia ni kuunganisha kwenye gridi ya taifa kutoka Mbeya - makete na sasa zoezi hilo lipo ukingoni hivyo wananchi wawe na subira kidogo kwa kuwa linawezekana

Na Veronica Mtauka, Makete


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo