Jeshi la Polisi katika Mkoa wa Kipolisi Tarime/Rorya limefanikiwa kumuua
jambazi sugu baada ya jambazi huyo kupambana na askari wa jeshi hilo
kwa kurushiana risasi katika kitongoji cha Ntarechagini kijiji cha
Nyamwaga Wilaya ya Tarime Mkoani Mara.
Kamanda wa polisi katika Mkoa wa Kipolisi Tarime /Rorya Kamishina msaidizi Justus Kamgisha amesema baada ya jeshi hilo kupata taarifa kutoka kwa raia mwema na kuanza kumfuatilia jambazi huyo ndipo risasi zilianza kurushwa kutoka kichakani na kisha Polisi hao kujibu na kufanikiwa kumpiga Jambazi huyo.
Kamanda Kamgisha amemtaja jambazi huyo kuwa ni Senso Magabe Mwita ambaye alikuwa akitafutwa na Jeshi hilo kwa Makosa mbalimbali likiwemo la Mauaji, unyang’anyi wa kutumia silaha likiwemo tukio la Mauaji lililotokea Desemba 30 na alikuwa na tabia ya kuleta majambazi toka nchi jirani ya Kenya.
Kamanda wa polisi katika Mkoa wa Kipolisi Tarime /Rorya Kamishina msaidizi Justus Kamgisha amesema baada ya jeshi hilo kupata taarifa kutoka kwa raia mwema na kuanza kumfuatilia jambazi huyo ndipo risasi zilianza kurushwa kutoka kichakani na kisha Polisi hao kujibu na kufanikiwa kumpiga Jambazi huyo.
Kamanda Kamgisha amemtaja jambazi huyo kuwa ni Senso Magabe Mwita ambaye alikuwa akitafutwa na Jeshi hilo kwa Makosa mbalimbali likiwemo la Mauaji, unyang’anyi wa kutumia silaha likiwemo tukio la Mauaji lililotokea Desemba 30 na alikuwa na tabia ya kuleta majambazi toka nchi jirani ya Kenya.
