![]() |
| Mabasi ya mwendo kasi 2014 kimara kivukoni. Picha kwa hisani ya Deo Mutta Mwanatanga |
Mtendaji mkuu wakala wa mradi wa mabasi yaendayo haraka Bi Asteria
lambo amesema basi hilo ni miongoni mwa mabasi madogo yatakayoingia
nchini yenye uwezo wa kubeba zaidi ya abiria 40 na makubwa yatabeba
abiria zaidi ya 150 na kuwataka wakazi wa jiji la Dar es Salamu
kuendelea kuwa na subira na kuwahakikishia mradi huo sio ndoto na adha
ya usafiri itapungua mapema mwaka kesho.
Nao baadhi ya wakazi wa jiji walioshuhudia gari hilo wameelezea
kufurahishwa na kuanza kuwa na imani na serikali yao ambapo wamesema
kama mradi huo utakamilika kwa muda uliopangwa utakuwa faraja sana
kutokana na adha kubwa ya usafiri wanayokumbana nayo huku wakitoa wito
kwa mamlaka husika kupanga mikakati ya kupunguza nauli za mabasi hayo
pindi yatakapoanza kufanya safari zao.
ITV


