Shirika la umeme nchini TANESCO limetangaza rasmi kuanza kwa mgawo wa umeme kuanzia kesho Jumamosi Novemba 16.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, afisa uhusiano wa TANESCO Bi Badra Masoud amesema mgawo huo utahusisha mikoa yote iliyounganishwa na gridi ya taifa
Amesema sababu ya kuanza kwa mgawo huo ni kutokana na kupungua kwa gesi kutokana na matengenezo yanayoendelea katika vinu vya gesi huko Songosongo mkoani Lindi
