Hali
ya wanawake inazidi kuwa mbaya ndani ya nchi yao inayosifiwa kuwa ni
Kisiwa cha Amani (Amani kwa wanaume) Tukio hili lilitokea mapema mwezi
wa nane mwaka huu. Katika mazungumzo yake huyu binti alisema kwamba
anatamani sana kurudi nyumbani kwa wazazi wake, tatizo ni kwamba kwa
kuwa alilipiwa mahari na mume wake (aliyemkata panga mguu na kuutoa)
hawezi kurudi wala mama hawezi kumkubalia arudi kwao ni mpaka baba yake
aje atoe ruhusa ya yeye kurudi nyumbani. (mbayaaaaa, sanaaaa.
anajisemeaga Mch Rwakatare)
Samahani
kwa picha mbaya, lakini hatuna budi kuonyesha unyama uliopita kipimo
ambao wanawake wanaupitia. juu ni kipande cha mguu wa huyo binti ambao
mume alipitisha panga mithili anakata muwa( Kumbuka tupo kwenye
maandalizi mazito ya kuandimisha siku 16 za kupinga ukatili dhili ya
Wanawake)
Mama
mzazi wa binti aliyekatwa mguu na mkwe wake akilia kwa uchungu mkubwa
alipokuwa anaelezea kisa kilichomkumba binti yake. Ni huzuni kubwa sana
ukivaa viatu vya familia hii. Mama anasema kwa utamaduni wao baba wa
mtoto aliyekatwa yaani mume wake ndiye mwenye dhamana ya kuamua mtoto
arudi nyumbani au aendelee kubaki ka mume fedhuli aliyemgeuza mwenzake
ni pingili la muwa.
Juu
ni mama na chini ni binti akiwa na mawazo juu ya kupoteza mguu wake kwa
sababu tu mume kaamua kuukata. Huyu binti ameathirika sana kisaikolojia
kutokana na tatizo hilo la kukatwa mguu wake na mume wake. hivyo
anaomba asaidiwe arudi nyumbani kwa wazazi wake, au popote pa kuishi
ilimradi aondolewe kwenye mazingira yale aliyopatia mkasa huo. Mbaya
zaidi baba mkwe wake anamwambia "wewe unaona raha kulala kitandani
wakati mtoto wangu analala chini jela) kwa kauli hiyo huyu binti yupo
hatarini zaidi. wanaweza kumuua wapoteze ushaidi. hata hivyo binti
aligusia sababu ya kufanyiwa unyama huo ni mwanaume kuwa na mwanamke
mwingine na kwamba alishahamishia mapenzi huko, na kumuona yeye kama
dudu mtu. (Wakati tunaendelea na maadhalizi ya siku 16 za kupinga
ukatili dhidi ya Wanawake, bado hali ni tete)
Hawa
ndio Washika dau wetu wakubwa serikalini. wanasimamia Wizara ya Jinsia
Maendeleo ya Jamii na Watoto. jamani waheshimiwa sana mko wapi? huku
wanawake twafaaa, mnatusaidia vipi? viti vya bunge vinakalika vipi kwa
hali hii? ni lini wanawake tutapaza sauti zetu ili dunia ijue unyama huu
unaoendelea dhidi ya wanawake wa Tanzania? Wanawake Hatuna AMANI kabisa
ndani ya nchi yetu.
Wizara na Taasis mbalimbali, Wadau wa kutokomeza ukatili dhidi ya
Wanawake, kuna jinsi ya kumsaidia huyu mama kwa kumuondoa pale kwenye
ile nyumba na akapewa makao salama?
Usikose kufuatilia Joyce Kiria Wanawakelive EATV na hapa kwenye ukurasa
wetu, ili upate mkasa huu wakati tunajipanga kuendelea na mapambano ya
Ukatili wa Kijinsia dhidi ya Wanawake.
PICHA KWA HISANI YA WANAWAKELIVETV.COM