Mgeni
rasmi katika hafla hiyo ya kukabidhi tuzo ya Daudi Mwangosi Bw Tido
Mhando wa tatu kulia akimkabidhi mshindi mfano wa hundi ya Tsh
milioni 10 Absalom Kibanda tuzo yenye thamani ya Tsh milioni 10,0000
katikati ni mjane wa Mwangosi Itika Mwangosi wa kwanza kushoto ni
makamu wa rais wa UTPC Jane Mihanji na rais wake Keneth Simbaya. ======= MHARIRI Mtendaji wa
New Habari 2006 Ltd. Absalom Kibanda ameibuka mshindiwaTUZO ya uandishi
wa kishujaa na utumishi uliotukuka ya Daudi Mwangosi iliyoandaliwa na
Muungano wa Klabu za waandishi wa Habari nchini (UTPC) na kujipatia
kiasi cha shilingi milioni 10.
Kibanda
alitangazwa leo Jijini Mwanza na Jopo la Majaji walioteuliwa kufanya
mchakato wa kumtafuta mwaandishi wa Habari bora kwa mwaka huu kwenye
hafla fupi katika Hoteli ya JB Belamont na kuhudhuliwa na Wahariri wa
Vyombo vya Habari, viongozi wa UTPC,Viongozi wa Klabu za Waandishi wa
Habari nchini , Wanahabari na Wageni mbalimbali zaidi ya 120 kutoka
ndani na nje ya Tanzania' Mjumbe wa Kamati ya
Majaji hao Hamza Kassongo kwa idhini ya Mwenyekiti wake Nkwabi
Mwanakilala alisema kwamba Jopo la Majaji lilitembea Mikoa mbalimbali
nchini kupita na kufanya utafiti kwa waandishi wa habari na wahariri
wanaotekeleza majukumu yao kwa ufasaha zaidi na kupambana na vitendo vya
udhalilishaji na unyanyasaji kutoka kwa viongozi wa serikali, wanasiasa
na makundi mbalimbali ikiwa ni lengo la kuwatisha waandishi hao.
Kassongo
aliwataja majaji wengine wanne ambao walitumia muda kufanya uchambuzi
wa kumpata mshindi kuwa ni pamoja na Nkwabi Mwanakilala (Mwenyekiti),
Hamza Kassongo, Leila Sheikh, Dr. Ayoub Ryoba na Rosemary
Mwakitwange(wote wakiwa wajumbe wa jopo la majaji ambao wametekeleza
majukumu yao baada ya kuteuliwa na Bodi ya Wakurugenzi wa UTPC kufanya
kazi hiyo kwa uadilifu na kufuata vigezo vilivyowekwa.Msemaji wa jopo hilo la Majaji hao
aliongeza kuwa mshindi wa Tuzo hiyo ambaye ametangazwa amekidhi vigezo
na hakuna uchakachuaji na wakubaliane na uamuzi wa jopo hilo na kisha
alimwomba Leila Sheikh kupita mbele kumtangaza mshindi wa Tuzo hiyo
ambapo alimtangaza Kibanda kuwa mshindi wa waandishi wa habari nchini
kwa mwaka huu baada ya kushinda vigezo kumi viliyoainishwa..
| |