skip to main |
skip to sidebar
MAKAMU WA RAIS DK BILAL AKIRI KUWEPO KWA UHABA WA WAALIMU NA WATAALAM WA SAYANSI NCHINI
Serikali
imekiri kuwa bado kuna uhaba mkubwa wa walimu na wataalam wa masuala ya
sayansi nchini na kuongeza kuwa kuna haja ya kubuni mbinu mpya
zitakazojenga mazingira ya kuwavutia wanafunzi kusoma masomo hayo na
walimu wa masomo hayo kuwa na moyo zaidi wa kufundisha.
Makamu wa Rais Dk Mohamed Ghalib Bilali ameyasema hayo muda mfupi baada
ya kufungua rasmi jengo la kituo cha walimu lililopo chuo kikuu
kishiriki cha Elimu DUCE kilichopo Chang'ombe jijini Dar es salaam,
jengo lililojengwa ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa awamu ya kwanza ya
mradi wa sayansi, teknolojia na elimu ya juu uliotekelezwa na benki ya
dunia kwa kipindi cha miaka mitano na kushirikisha taasisi za elimu ya
juu kumi na tano.
Makamu wa rais amesema pamoja na hitaji kubwa
la walimu wa sekondari na vyuo vya elimu ya juu, hadi sasa takwimu
zinaonyesha kuwa asilimia ishirini ya walimu wanaofundisha sekondari
nchini ndio wenye degree huku uhaba wa walimu wa sayansi ktika shule
hizo ukiwa ni 25,000.
JIUNGE NA EDMO BLOG SASA
Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube
Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi