PICHA ZA MAZISHI YA MEJA MSHINDO ALIYEUAWA CONGO DRC

Wapiganaji wa Jeshi la Wananachi wa Tanzania { JWTZ } wakitoa salamu zao za mwisho wakati wa mazishi ya kamanda wao Meja Khatibu Shaaban Mshindo yaliyofanyika kijijini kwake Mangapwani.

Meja Khatib Shaaban ambae alikuwa Mkuu wa Kambi ya Kibaha alifariki dunia Mjini Goma Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo akiwa katika ulizi wa amani katika kikosi cha kulinda amani cha Umoja wa Mataifa.
Mamia ya wananachi, ndugu na Jamaa walioshiriki kuusitiri mwili ma marehemu Meja Khatibu Shaaban katika mahali pake Huko Mwangapwani Wilaya ya Kaskazini B, Mkoa wa Kaskazini Unguja.
Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akiongoza mamia ya wanajeshi, wananchi na Ndugu  na jamaa katika Mazishi ya Meja wa Kikosi cha JWTZ  Kibaha Khatib Shaaban aliyeuawa Nchini DRC akiwa katika shughuli za ulinzi wa vikosivya Umoja wa Mtaifa.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mohammed Aboud Mohammed akitia udongo kwenye kaburi wakati wa mazinshi ya Meja Khatibu Shaaban Mshindo yaliyofanyika kijijini kwake Mangapwani.
Mwakilishi wa Vikosi vya Umoja wa Mataifa vilivyopo Mjini Goma Nchini Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo Meja E.B. Samuel akitia udongo kuashiria ushiriki wa Umoja wa Mataifa katika mazishi ya  Marehemu Meja Khatibu Shaaban Mshindo yaliyofanyika kijijini kwake Mangapwani.

Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akimfariji Kiongozi wa Familia ya Marehemu Meja Khatibu Shaaban Mshindo bwana Alhaji Machano Mtumweni mara baada ya kukamilika kwa mazishi ya Kamanda huyo yaliyofanyika kijiji kwake Mangapwani Mkoa wa Kaskazini Unguja.

Picha na Hassan Issa wa – OMPR – ZNZ.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo