KAMATI YA UONGOZI NA KAMATI YA KANUNI YA BUNGE ZAKUTANA KUJADILI SAKATA LA TAZARA

Kamati ya uongozi na kamati ya kanuni ya bunge zimelazimika kukutana kwa dharura bungeni mjini Dodoma baada ya baadhi ya wabunge kuomba muongozo wa spika kusitisha shughuli nyingine za bunge ili kulijadili suala la mgogoro wa wafanyakazi wa Tazara  kwa madai kuwa mgogoro huo unaathiri uchumi wa nchi na jamii kwa ujumla.

Naibu spika wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Job Ndugai ndiye aliyeamuru kamati hizo kukutana kwa ajili ya kulijadili suala hilo na kulitoloea maamuzi baada ya mh suzan kiwanga mbunge wa chadema kusimama kwa mujibu wa kanuni ya bunge ya 47 na 48 kulitaka bunge kusitisha shughuli nyinginezo na kulijadili suala la mgogoro wa wafanyakazi wa Tazara.

Waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu sera,uratibu na bunge Mh William Lukuvi akasimama ambapo licha ya kukiri kuwepo kwa tatizo hilo amedai kuwa mejimenti na bodi ya Tazara inahusisha nchi mbili za Tanzania na zambia na kwamba serikali ya tanzania haiwezi kutoa maamuzi bila ya kuihusisha serikali ya zambia na kwamba suala hilo linaendelea kushughulikiwa  

Majibu hayo ya Mh lukuvi yakamlazimisha mnadhimu mkuu wa kambi ya upinzani bungeni Mh Tundu Lisu kusimama na kumtaka naibu spika kutoa uamuzi juu ya suala hilo kwa kuwa bunge si serikali
 
CHANZO:ITV


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo