Wafanyabiashara
zaidi ya 2000 wa soko kuu la Majengo Manispaa ya Dodoma wametishia
kutolipa ushuru kuanzia Septemba mosi mwaka huu kwa madai kuwa Manispaa
ya Dodoma imeshindwa kutatua kero za muda mrefu zinazowakabili ikiwemo
uchakavu wa miundombinu, ukosefu wa vyoo na kushindwa kudhibiti
wafanyabiashara holela katika maeneo yasiyo rasmi.
Hayo
yamesemwa na Mwenyekiti wa umoja wa wafanyabiashara hao Godson Rugazama
ambaye anasema licha ya kupeleka madai yao mara kwa mara kwa uongozi wa
Manispaa ya Dodoma bado hayafanyiwi kazi
SOURCE:ITV