POLISI WATAWANYA MAANDAMANO YA WAKULIMA TARAFA YA TURIANI MOROGORO


Jeshi  la polisi mkoa wa Morogoro limezima maandamano na kuwatawanya kwa mabovu ya machozi na risasi za mipira wakulima wa vijiji vya  kisara tarafa ya Turiani wilayani Mvomero mkoani Morogoro  waliokuwa wakipinga wafugaji kuingiza mifugo katika mashamba ya wakulima.

Malalamiko hayo ya wakulima yamekuja kufuatia tukio la ngombe za wafugaji kuuawa ambapo wakulima hao wametupia lawama jeshi la polisi kushindwa kuondoa mifugo katika maeneo ya wakulima kama ilivyoagizwa na serikali ya wilaya na kuwatuhumu askari kutumia nguvu kutawanya maandamano na baadhi ya wakulima kushikiliwa na jeshi la polisi.

Akizungumzia tuhuma hizo mkuu wa kituo cha polisi Turia Rajab Shemndolwa amesema wamelazimika kutumia nguvu kutokana na wananchi kutofuata taratibu za kufanya maandano na kukaidi amri ya jeshi na kwa kufunga barabara kwa mawe kwa zaidi ya masaa manne na kuzuia shughuli za usafiri.

Nae mkuu wa wilaya ya Mvomero Antony Mtaka akizungumzia tuki hilo amekiri uharibifu mkubwa uliofanywa baada ya mahindi kuliwa na mifugo  hali inayosababisha njaa kwa wakulima waliolima lakini kuwa mkakati wa serikali sasa ni kusikiliza malamiko ya pande zote mbili katika kutatua mgogoro huo.

CHANZO:ITV


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo