POLISI-3
Kamanda wa polisi mkoa wa Singida ACP Geofrey Kamwela, akishiriki kufanya usafi katika kituo cha zamani cha mabasi mjini Singida ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya sku ya polisi nchini.
POLISI-2
Kamanda wa polisi mkoa wa Singida ACP Geofrey Kamwela, (wa pili kulia) akishiriki kufanya usafi katika kituo cha mabasi cha zamani, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya siku ya polisi nchini. Wa pili kushoto (aliyeinama) ni RCO mkoa wa Singida Thobias Sedoyeka, akishiriki kuzoa taka ngumu ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya siku ya polisi nchini.
POLISI-1
Afisa upelelezi mkoa wa Singida Thobias Sedoyeka, akishiriki kufanya usafi katika kituo cha zamani cha mabasi mjini Singida, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya siku ya polisi nchini.(Picha zote na Nathaniel Limu via mo blog).

Na Nathaniel Limu.
Jeshi la polisi mkoani Singida limeazimisha siku ya polisi nchini kwa kufanya usafi katika kituo cha zamani  cha mabasi  mjini Singida.

Akizungumza na Mo blog, Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Singida ACP Geofrey Kamwela, amesema wameamua kuadhimisha siku hiyo muhimu kwa jeshi la polisi kwa kusafisha mazingira eneo la kituo cha mabasi ili pamoja na mambo mengine, kuondoa uwezekano wa kutokea kwa magonjwa ya mlipuko.

Akifafanua amesema kuwa mazingira yakiwa machafu, yanasababisha madhara mengi ikiwemo kuficha

Amesema mazingira machafu yanachangia kutokea kwa milipuko ya magonjwa yanayoweza kusababisha  wananchi wasiweze kujiletea maendeleo endelevu.

Kwa hali hiyo, Kamanda Kamwela, ametoa wito kwa wakazi wote wa mkoa wa Singida wakiwemo askari polisi, kuhakikisha mazingira yanayozunguka makazi yao, yanakuwa safi wakati wote.


Aidha, amesema katika maadhimisho hayo, pia watayatumia  katika kujitathmini utendaji wao.

Amesema baada ya tathimini hiyo, watajiwekea  mikakati ya kuboresha utendjai wa kila siku, ili mkoa wa Singida, uendelee kuwa na amani na utulivu zaidi.