Habari za kusikitisha ambazo zimetufikia hivi punde zinasema jumla ya
watu 13 wamefariki dunia usiku wa kuamkia hii leo huku 11 wakijeruhiwa
vibaya baada ya gari walilokuwa wakisafiria aina ya Toyota Hiace kutoka
kijiji cha Ngogwa wilayani kahama kwenda ushirombo mkoani Shinyanga
kugonga lori kwa nyuma usiku wa kuamkia hii leo.
Akizungumza na mwandishi wetu Reuben Mchome wa MCHOME BLOG
kaimu kamanda wa pilisi mkoani shinyanga kamishna msaidizi wa polisi
KIHENYA KIHENYA amesema chanzo cha ajali hiyo ni dereva gari lililokuwa
limewabeba abiria hao aina ya Toyota Hiace kuligonga kwa nyuma lori
lililokuwa limepaki pembeni kidogo ya barabara ambalo lilikua
limeharibika.
Watu watatu kati ya 11 waliojeruhiwa wapo mahututi katika hosiptali ya mkoa wa shinyanga na ni watu wanne tu waliotambuliwa kati ya 11 waliopoteza maisha katika ajali hiyo.
Watu watatu kati ya 11 waliojeruhiwa wapo mahututi katika hosiptali ya mkoa wa shinyanga na ni watu wanne tu waliotambuliwa kati ya 11 waliopoteza maisha katika ajali hiyo.
Chanzo:MCHOME BLOG
